Loading...
title : Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo
link : Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo
Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo
Na Karama Kenyynko, blogu ya Jamii
Uamuzi kama hakimu Hakimu Mkazi Mkuu ,Wilbard Mashauri anayeendesha kesi inayowakabili viongozi tisa wa Chadema waliomtaka ajitoe kusikiliza kesi hiyo utatolewa Julai 10, mwaka huu.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu itatoa uamuzi ambao itajulikana kama Hakimu Mashauri atajitoa ama la.
Uamuzi huo ulipaswa kutolewa leo Julai 5, 2018 na Hakimu Mashauri lakini umeahirishwa baada ya wakili wa utetezi Hekima Mwasipu kuieleza mahakama kuwa mawakili wa upande wa utetezi, Jeremiah Mtobesya na Peter Kibatala wanasikiliza kesi nyingine Mahakama Kuu,
Upande wa mashtaka katika kesi hiyo ya uchochezi unawakilishwa na mawakili wa Serikali, Faraja Nchimbi, Dk Zainabu Mango, Paul Kadushi na Wankyo Simon.
Akijibu hoja ya kutokuwepo mawakili wa utetezi wakili Nchimbi alieleza kuwa siyo busara uamuzi huo kutolewa bila ya kuwepo kwa mawakili wa utetezi lakini kwa kuwa wanaamini kesi za Mahakama Kuu husikilizwa asubuhi aliomba uamuzi huo utolewe nyakati za mchana ili mawakili hao waweze kuwepo.
Baada ya kusikiliza hoja za upande zote, hakimu Mashauri alikubaliana na Maelezo ya upande wa utetezi na kuiahirisha kesi hadi Julai 10, 2018 ambapo atatoa uamuzi kama atajitoa katika kesi hiyo ama la
Awali, mshtakiwa Freeman Mbowe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama hicho na wenzake nane waliieleza mahakama kuwa hawana imani na Hakimu huyo Mashauri anayeiendesha kesi hiyo na kila mmoja akieleza sababu zake na kumtaka ajitoe
Wakili Peter Kibatala awali akiwasilisha hoja Julai 2,2018, alidai kuwa wateja wake wamemueleza kuwa hawana imani naye na kwamba wanaomba ajitoe kusikiliza kesi hiyo.
Washtakiwa katika Kesi hiyo ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu na Naibu katibu Mkuu bara na Mbunge wa kibamba John Mnyika, mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, Mbunge wa Kawe Halima Mdee na mbunge wa bunda, Esther Bulaya.
Wengine ni katibu mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji, mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa, Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko.
Washtakiwa kwa pamoja wanakabiiwa na mashtaka 13, ambapo katika shtaka la kwanza la kula njama, kwa pamoja Februari 1 na 16, 2018, Dar es Salaam walikuĺa njama pamoja na wenzao ambao hawapo mahakamani walikula njama ya kutenda kosa la kufanya mkusanyiko usio halali, mkusanyiko wenye ghasia na kukiuka tamko kutawanyika.
Hivyo makala Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo
yaani makala yote Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/uamuzi-kama-hakimu-anayesikiliza-kesi.html
0 Response to "Uamuzi kama Hakimu anayesikiliza kesi ya viongozi dhidi ya viongozi wa Chadema kujitoa ama la, kujulikana wiki ijayo"
Post a Comment