Loading...
title : KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO.
link : KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO.
KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO.
Kamati ya Bunge zinazotarajiwa kuketi kuanzia Jumatatu Agosti 20 hadi 31 mwaka huu Jijini Dodoma kabla ya kuanza kwa mkutano wa kumi na mbili wa Bunge unaotarajiwa kuanza Septemba 4 mwaka huu.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kitengo cha Habari, Elimu kwa Umma na Mawasiliano Ofisi ya Bunge Dodoma imesema kkamati hizo zitakaa na kuchambua miswaada mbalimbali ya sheria kabla ya kuanza kwa mkutano huo wa 12.
Miongoni mwa Mswaada unatarajiwa kupitiwa ni pamoja na mswaada wa Sheria wa kuitangaza Dodoma kuwa Makao Makuu ya Nchi (Mswaada wa Sheria wa 2018) pamoja na miswaada mingine minne.
Katika hatua nyingine Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyeambatana na ujumbe wake wa uongoza wameendesha kikao cha mafunzo kwa kamati ya uongozi, makamu wenyeviti na wajumbe wa tume ya utumishi ya bunge yanayoendelea katika ofisi ndogo za Bunge, Zanzibar.
Aidha amapema, Ijumaa Spika wa Bunge, Job Ndugai pamoja na ujumbe wake huo ambao ni wawakilishi wa Kamati ya Bunge ya Uongozi na wawakilishi wa Tume ya Utumishi ya Bunge walimtembelea Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohamed Shein Ikulu, Zanzibar.
Hivyo makala KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO.
yaani makala yote KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO. mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/08/kamati-ya-bunge-kuanza-vikao.html
0 Response to "KAMATI YA BUNGE KUANZA VIKAO."
Post a Comment