Loading...
title : UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA
link : UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA
UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA
Na Karama Kenyunko, Blogu ya Jamii.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeelezwa kuwa upelelezi dhidi ya kesi ya mauji inayomkabili Mwanajeshi MT 109795 Private Ramadhan Mlaku (28) anayedaiwa kuumua askari mwenzie, MT 79512 SGT Saimon Munyama bado haujakamilika na inasubiliwa ripoti ya mtaalamu wa milipuko ili kukamilisha.
Hayo yameelezwa leo Agosti, 23.2018 na wakili wa Serikali Mwandamizi, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba shauri hilo lilipoitishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kutajwa.
Mwita amedai kuwa bado wanasubiri ripoti ya mtaalamu wa milipuko ili kukamilisha upelelezi wa kesi hiyo na kuongeza kwamba mawasiliano kidogo yamesumbua kuhusu baadhi ya vielelezo baina ya Jeshi la JWTZ na Polisi,
Baada ya taarifa hiyo, Hakimu Simba ameutaka upande wa mashtaka kuharakisha mchakato huo ili hatma ya kesi ijulikane na ameiahirisha kesi hiyo hadi September 6,2018 kwa ajili ya kutajwa.
Mshtakiwa huyo ambaye ni Mwanajeshi wa Kambi ya Jeshi Makongo anadaiwa kutenda kosa la mauaji October, 30, 2017 akiwa Makao Mkuu ya JWTZ Upanga Ilala Dar es Salaam ambapo alimuua askari mwenzie MT 79512 SGT Munyama.
Hivyo makala UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA
yaani makala yote UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/08/upelelezi-wa-kesi-ya-mauaji-ya.html
0 Response to "UPELELEZI WA KESI YA MAUAJI YA MWANAJESHI BADO HAUJAKAMILIKA"
Post a Comment