Loading...

WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA

Loading...
WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA
link : WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA

soma pia


WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA

 KAIMU Mganga  Mfawidhi wa Hospitali ya Wilaya ya Mkuranga  Mkoa  wa Pwani Ndaki Barnabas amethibitisha  kuwapokea  majeruhi watatu  ambao walijeruhuwa katika kata ya Bupu Wilayani Mkuranga na kundi la wafugaji  wanao sadikika kuwa ni kutoka jamii ya wamang'ati waliowavamia  jana jioni wakitokea katika eneo la Kisarawe Mkoani Pwani.

Dokta Ndaki amesema amewataja majeruhi hao kuwa ni  Leonard Kondo,  Mustafa Seif  na  Abdallah Rashid  waliopokewa hospitalini hapo na kupatiwa matibabu  majira ya saa nne usiku jana.

Dokta Ndaki anasema kuwa walipofikishwa hospitalini hapo hali za majeruhi hao zilikua mbaya na kuvuja damu lakini sasa wanaendelea vizuri baada ya kushonwa na kupata tiba ya awali huku akisema kuwa  Daktari wa zamu amepita na kutoa ruhusa kwa majeruhi wawili huku majeruhi mmoja  watampa rufaa ili aende kupata vipimo vya   XRay na kipimo cha Ultra Sound sababu ameumia kwenye maeneo ya ndani ya mwili ikiwemo  mbavuni na ana maumivu makali.
 Wakizungumza na globu ya jamii mchana huu wakiwa wodini wagonjwa hao wameelezea namna walivyovamiwa na kupigwa vibaya na wafugaji hao.


Akizungu huku akiwa kitandani  majeruhi Abdallah rashid  ambaye ni mkazi wa Mbagala amesema akuwa  yeye alikwenda Kisarawe kuwasalimia wakwe zake na kadhia hiyo ilimkuta wakati alipokwenda dukani kununua vocha ndipo ghafla  wakatokea  wamang'ati huku wakimuuliza kama ameonga ng'ombe aliyekatwa mguu akajibu hajaona ghafla wakamvamia na kuanza kumpiga  kwa kutumia gongo kichwani.

"Nikawaona wenyeji wanakimbia  na mimi nikaona hapo sasa kuna hatari nikakimbia nankwenda kujificha kwenye nyumba nikapata akili ya kumpigia Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Pwani lkn akasema yeye hivi sasa ameshahamishwa hivyo akaniambia nimpigie RPC mpya wa sasa nikafanya hivyo Kamanda wa sasa alipokea simu na kuniambia ndani ya nusu saa askari watakuwa wamefika kutuokoa kweli walifika ndani ya muda na wakatuchukua kutupeleka hosputali" anasema  majeruhi huyo.


Tukio limethibitishwa na Mkuu wa Wilaya ya Mkuranga  Philiberto Sanga huku akiahidi kuwa kesho ataambatana na Kamati ya Ulinzi ya Wilaya ya Mkuranga  kwenda katika eneo la tukio.

Aidha Mkuu huyo wa Wilaya amewataka Madiwani na wananchi waanzishe daftari la kuwaandika wageni wanaoingia nankutoka katika maeneo yao ili kudhibiti vitendo viovu.


Hivyo makala WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA

yaani makala yote WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/08/wamangati-wawajeruhi-watatu-mkuranga.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAMANG'ATI WAWAJERUHI WATATU MKURANGA"

Post a Comment

Loading...