Loading...
Loading...
- Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa , tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title :
link :

soma pia


NA MWAMVUA MWINYI, PWANI 
WIZARA ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi 
imeziasa halmashauri kuhakikisha zinapima maeneo ya wananchi na kuyaingiza kwenye mfumo ili kutambua idadi ya viwanja na mashamba wanayopaswa kulipa na kupatiwa hati miliki. 

Imetoa rai kwa halmashauri hizo kutotumia kigezo cha kutopewa fedha na wizara hiyo kwa ajili ya bando la kuweka katika mfumo kama kikwazo cha kushindwa kukusanya mapato yatokanayo na ardhi.

Hayo yalisemwa mjini Kibaha na Naibu Waziri wa Wizara hiyo Angeline Mabula.

Alisema , suala hilo ni aibu kwa halmashauri kudai wanakosa kiasi cha sh. 20,000 ama 30,000 ya vocha .

Angeline alieleza, halmashauri wasigeuze jambo hilo kama ni changamoto ya kushindwa kukusanya mapato yatokanayo na ardhi na kusubiri kupewa na wizara wakati hilo liko ndani ya uwezo wao.

“Mnakusanya mabilioni ya fedha kupitia viwanja mnashindwaje kukusanya mkiwa mnasubiri vocha ya shilingi 20,000 au 30,000 hili halikubaliki "

Angeline alifafanua,, halmashauri zihakikishe zinawezesha idara ya ardhi iweze kukusanya mapato badala ya kuiacha kama mtoto yatima .

“Tumerejesha maeneo mengi lakini nia njema ya kufanya hivyo baadhi halmashuri zimekiuka mnaweza kuwa na kasi ya kutaka maendeleo lakini unapaswa kufuata taratibu hatuwezi kutoa maeneo bila kufuata taratibu,” alisema Angeline. 

Ofisa ardhi mteule wilaya ya Kibaha ,Majaliwa Jafari alieleza viwanja 1,700 vimepimwa lakini havijauzwa ambapo Kisabi 800 Disunyala 700 .

Awali akisoma taarifa ya wilaya katibu tawala wa wilaya hiyo Sozi Ngate alisema , halmashauri ya wilaya ilikusanya milioni 504 na kutoa hatimiliki za kimila na imepima vijiji 22.

Anasema, mpango shirikishi wa matumizi bora ya ardhi umegusa maeneo tisa kati 25 vilivyopo ikiwemo Lukenge, Gumba, Magindu, Mpiji Station, Kwala, Dutumi, Minazimikinda, Mperamumbi.
 Mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama akizungumza wakati Naibu Waziri wa wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ,Angeline Mabula alipofanya ziara ya siku moja wilayani Kibaha.
 Mbunge wa Kibaha Vijijini, Hamoud Jumaa akieleza jambo, wakati Naibu Waziri wa wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ,Angeline Mabula alipofanya ziara ya siku moja wilayani Kibaha.
Naibu Waziri wa wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi ,Angeline Mabula ( wa katikati) akimsikiliza mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Assumpter Mshama (wa kwanza kulia )wakati alipofanya ziara ya siku moja wilayani Kibaha, (wa kwanza kushoto) ni mbunge wa Kibaha Vijijini Hamoud Jumaa.
(Picha na Mwamvua Mwinyi) 


Hivyo makala

yaani makala yote Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/09/na-mwamvua-mwinyi-pwani-wizara-ya-ardhi.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to " "

Post a Comment

Loading...