Loading...
title : MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'.
link : MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'.
MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'.
Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Dkt Sinare Yusuph Sinare akimkabidhi rasmi Uenyekiti wa Baraza hilo Bi Jacqueline Mkindi baada ya kuteuliwa na Bodi na kuthibitishwa na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania, Dkt Sinare amemaliza muda wake baada ya kushika nafasi hiyo kwa kipindi cha miaka 5.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akizungumza na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania baada kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi, kushoto kwake ni Makamu Mwenyekiti Mh Jitu Son na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Tanzania Bi Janeth Bitegeko, Mkutano huo umefanyika Jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akimkabidhi tuzo ya heshima ya utendaji uliotukuka katika Sekta ya Kilimo, Mwenyeki wa Bodi ya Baraza la Kilimo aliyemaliza muda wake Dkt Sinare Yusuph Sinare , kati kati ni Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Kilimo Bi Janeth Bitegeko, tukio hilo limefanyika Dar es Salaam wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania.
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi akimakabidhi tuzo ya heshima ya utendaji uliotukuka katika Sekta ya Kilimo, Mwenyeki wa Taasisi ya Sekta Binafsi Nchini ambaye pia ni mjumbe wa bodi ya baraza la kilimo Bw Salum Shamte, tukio hilo limefanyika Dar es Salaam wakati wa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo Tanzania

Wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Mh Jitu son ambaye kwa sasa ni Makamo Mwenyekiti wa Baraza la Kilimo Tanzania, na Bw Julias Nyabicha wakifuatilia kwa makini kitabu cha mahesabu wakati wa Mkutano Mkuu wa wajumbe wa Baraza la Kilimo Tanzania uliofanyika Dar es Salaam, wengine kwenye picha ni sehemu ya wajumbe wa Mkutano huo.

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania Bi Jacqueline Mkindi, kulia ni makamo wake Mh Jitu Son, kushoto ni mwenyekiti aliyemaliza muda wake Dkt Sinare Yusuph Sinare wakiwa kwenye picha na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi ya Baraza la Kilimo Tanzania muda mfupi baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa Baraza la Kilimo uliofanyika Dar es Salaam.
Hivyo makala MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'.
yaani makala yote MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'. mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/11/mwenyekiti-mpya-bodi-ya-wakurugenzi.html
0 Response to "MWENYEKITI MPYA BODI YA WAKURUGENZI BARAZA LA KILIMO TANZANIA AKABIDHIWA 'KIJITI'."
Post a Comment