Loading...
title : BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA
link : BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA
BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA
ZAIDI ya wakulima 1,032 wameanza kutumia Teknolojia ya Kilimo Hifadhi inayomuwezesha mkulima kukabilaina na mabadiliko ya tabia nchi ikiwa ni pamoja na kupata mavuno mengi zaidi tofauti na Kilimo cha mazoea cha kutegemea Mvua Pekee.Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa mradi wa ubia wa kilimo Tanzania mwaka 2018 ulio chini ya baraza la kilimo Tanzania imesema wakulima hao ni kutoka Wilaya za Same, Moshi Vijini, Babati, Monduli na Kiteto ambapo wakulima zaidi ya 2500 walipata mafunzo kuhusu kilimo hifadhi.
Hayo yalielezwa na Mratibu Taifa wa Ubia wa Kilimo Tanzania Mark Magila wakati alipokuwa akizungumza na wajumbe waliohudhulia Warsha ya wadau TAP II iliyofanyika mwishoni mwa wiki Wilayani Kyela Mkaoni Mbeya ambapo aliwaeleza kuwa teknlojia hiyo inamsaidia mkulima kupata mavuno mengi huku akitumia sehemu ndogo ya ardhi.
“Mpaka sasa TAP II tumekwisha fanikiwa kutoa mafunzo ya stadi za kilimo biashara kwa wakulima 700 kutoka kwa wilaya 7 za Meru, Kiteto, Babati, Kilombero, Morogoro Vijijini, Namtumbo na Songea Vijijini lengo ikiwa ni kuendelea kuwajengea uwezo wakulima nchini, “Lakini pia AMCO 20 zilijengewa uwezo juu ya masuala ya mikopo na kuwaunganisha na watoa huduma za kifedha kwenye wilaya 10 ambazo ni Sumbawanga, Mpanda, Kyela, Mvomero, Morogoro Vijijini,Kilombero, Ulanga, Mufindi, Iringa na Mbeya” ilisema taarifa hiyo iliyosomwa na Mark Magila mratibu wa taifa wa TAP II.
Mratibu wa Taifa wa Ubia wa Kilimo Tanzania Mark Magila akitoa taarifa ya utekelezaji wa shughuli za TAP II kwa Mwaka 2018 kwa wajumbe waliohudhulia warsha ya wadau wa TAP iliyofanyika mwishoni mwa wiki Wilayani Kyela Mkaoni Mbeya.
Afisa Masoko wa Ubia wa KIlimo Tanzania Alinanuswe Ambalile aakiwasilisha mada kwa wajumbe waliohudhulia warsha ya wadau wa TAP kuhusu mnyororo wa thamani kwenye mazao.
Mwakilishi wa Ubia wa kilimo Tanzania kwa ZONE 1 yenye mikoa ya katavi, songwe na rukwa, Wilson Ernest Loth (wa pili kulia) akiwa na wadau wengine wa TAP wakifuatilia warsha ya wadau wa TAP iliyofanyika mwishoni mwa wiki Wilayani Kyela Mkaoni Mbeya.
Sehemu ya washiriki wa warsha ya siku moja ya wadau wa TAP iliyifanyika mwishoni mwa wiki Wilayani Kyela Mkaoni Mbeya.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA
yaani makala yote BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/baraza-la-kilimo-tanzania-lafanya.html
0 Response to "BARAZA LA KILIMO TANZANIA LAFANYA MKUTANO WAO MKOANI MBEYA"
Post a Comment