Loading...

Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina

Loading...
Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina
link : Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina

soma pia


Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina

Na Mwandishi wetu
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP Dr Reginald Mengi amewaalika wafanyabiashara kutoka China washirikiane naye kuwekeza nchini kwa ubia katika miradi mbalimbali, wakati huu  ambapo Tanzania inapojizatiti kuwa ya viwanda.
Dr Mengi ametoa rai hiyo jijini Dar es salaam wakati wa chakula cha mchana alichowaandalia  wawakilishi wa makampuni   17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji, walioambatana kwenye hafla hiyo na Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke.
Amesema Tanzania ni nchi iliyojaaliwa fursa nyingi za uwekezaji kutokana na utajiri wake wa  raslimali na kusisitiza kuwa waliotayari kushirikiana naye katika miradi mbalimbali kama ya ujenzi wa bomba la gesi kutoka Tanzania hadi Uganda wajitokeze.
Akizungumza katika hafla hiyo Balozi wa China nchini  Mhe. Wang Ke amesema ofisi yake itakuwa kiunganishi  baina ya Wafanyabiashara wa China na Dr Mengi katika kufanikisha pendekezo la kuanzisha kwa ubia hapa nchini viwanda mbalimbali.
Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara hao Bw. Lyu Xinhua amesema amekuja na ujumbe kutoka makampuni 17 ya China yanahusika na shughuli mbalimbali kuanzia ujenzi wa miundombinu, uhandisi, teknolojia ya mawasiliano nk, na kuahidi kuwasilisha mapendekezo yaliyotolewa kwa makampuni husika kwa ajili ya hatua zaidi za utekelezaji.
 Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi akizungumza wakati wa chakula cha mchana alichowaandalia wawakilishi wa makampuni   17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Uanachama wa Tanzania Private Sector Foundation (TPSF), Bw. Louis Accaro, Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua, Balozi wa China nchini  Mhe. Wang Ke, Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha pamoja Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe.
 Balozi wa China nchini Mhe. Wang Ke akizungumza machache kabla ya kumkaribisha Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua kutoa salamu wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa wawakilishi wa makampuni   17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Wengine katika picha ni  Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa  IPP Touchmate, Bw. Victor Tesha (wa pili kulia) pamoja Msaidizi wa Dk. Mengi, Bw. Godfrey Bitesigirwe (kulia).
 Kiongozi wa Ujumbe wa wafanyabiashara kutoka China, Bw. Lyu Xinhua akitoa salamu kwa niaba ya ujumbe huo wakati wa chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi kwa wawakilishi wa makampuni   17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji katika hafla fupi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dr. Reginald Mengi


Sehemu ya wafanyabiashara wawakilishi wa makampuni  17 kutoka China waliopo nchini kutafuta fursa za uwekezaji waliposhiriki hafla fupi ya chakula cha mchana kilichoandaliwa Dr. Mengi iliyofanyika Serena Hotel jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina

yaani makala yote Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/dk-mengi-afungua-milango-ya-ushirikiano.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Dk Mengi afungua milango ya ushirikiano na wawekezaji wa Kichina"

Post a Comment

Loading...