Loading...

Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli

Loading...
Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli
link : Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli

soma pia


Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli


Na Greyson Mwase, Lindi

Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa Nchini wametakiwa kuongeza ubunifu kwenye ukusanyaji wa mapato ili kuweza kufikia lengo lililowekwa na Serikali hivyo Sekta ya Madini kuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 13 Desemba, 2018 na Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo kwenye kikao chake na watumishi wa Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Lindi iliyopo Wilayani Nachingwea mkoani Lindi ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku mbili kwenye mkoa huo, yenye lengo la kukagua shughuli za uchimbaji wa madini pamoja na kutatua kero mbalimbali.

Naibu Waziri Nyongo aliyekuwa ameambatana na Mkuu wa Wilaya ya Nachingwea, Rukia Mhango alisema kuwa, Serikali kupitia Wizara ya Madini imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha kuwa Sekta ya Madini inakuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa sekta nyingine kutokana na makusanyo ya kodi mbalimbali za madini.

“Ninawaagiza maafisa madini wakazi kuhakikisha wanafikia lengo lililowekwa na Serikali kwenye ukusanyaji wa kodi mbalimbali zitokanazo na Sekta ya Madini kwa kuwa wabunifu, na tupo tayari kusaidia pale itakapowezekana,” alisema Naibu Waziri Nyongo. 

Mtaalam kutoka kiwanda cha kuzalisha saruji cha Dangote kilichopo mkoani Mtwara, Victor Kamuhabwa (wa kwanza kulia mbele) akimwonesha Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto mbele) namna mfumo wa uendeshaji wa mitambo unavyofanya kazi kwenye ziara ya Naibu Waziri Nyongo kwenye kiwanda hicho tarehe 13 Desemba, 2018. 
Mtaalam kutoka kiwanda cha kutengeneza vyombo vya ibada kwa kutumia madini ya mawe kinachomilikiwa na Shirika la Benedictine Abbey katika Wilaya ya Masasi mkoani Mtwara, Mhandisi Kassari Viater (kulia mbele) akielezea namna mashine ya kukata mawe makubwa inavyofanya kazi kwa Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (katikati mbele) kwenye ziara ya Naibu Waziri Nyongo kwenye kiwanda hicho. 
Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Lindi, Sophia Omari (kulia) akibadilishana mawazo na Mhandisi Migodi Mwandamizi kutoka Ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mtwara, Aidan Gumbo Mhando (kushoto) kwenye ziara hiyo. 



Hivyo makala Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli

yaani makala yote Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/maafisa-madini-watakiwa-kuwa-wabunifu.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Maafisa Madini Watakiwa kuwa Wabunifu, Ukusanyaji Maduhuli"

Post a Comment

Loading...