Loading...
title : Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja
link : Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja
Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja
Taasisi za Umma zimeshauriwa kuwa na akaunti za makusanyo kwenye benki zaidi ya moja kati ya benki zilizoungwa na Mfumo wa Serikali wa Ulipaji wa Kielektroniki (GePG) ili kuwarahisishia walipaji wa huduma za serikali.
Ushauri huo umetolewa leo jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango wakati akifungua mkutano wa mwaka wa watumiaji wa mfumo wa GePG katika ukusanyaji wa fedha za umma uliozishirikisha taasisi za Umma zinazotumia Mfumo huo pamoja na timu ya GePG kwa ajili ya kujengeana uwezo wa namna bora ya kutumia mfumo huo.
Dkt. Mpango amesema kuwa utaratibu wa malipo kupitia GePG unatoa fursa ya kuwa na njia nyingi za kulipia fedha za umma pamoja na kuwapa walipaji wa huduma za serikali utaratibu rafiki na machaguo mengi ya kufanya malipo.
"Kwa kuwa malipo yote yanayopitia GePG hayatozwi ada za miamala na benki hizo hivyo kuongeza akaunti za makusanyo katika benki hakutoongeza gharama za miamala kwa taasisi za umma bali kufanya hivyo kutaondoa hatari ya Ofisi husika kukosa huduma ya malipo endapo benki inayotumika itashindwa kutoa huduma kwa sababu mbalimbali", alisema Dkt. Mpango.
Hivyo makala Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja
yaani makala yote Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/taasisi-za-umma-zashauriwa-kuwa-na_12.html
0 Response to "Taasisi za Umma Zashauriwa Kuwa na Akaunti za Makusanyo Kwenye Benki Zaidi ya Moja"
Post a Comment