Loading...
title : Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki
link : Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki
Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki
Na. Paschal Dotto-MAELEZO
Tanzania imeendela kuweka rekodi ya kuvutia wawekezaji kwa nchi zilizopo ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa na mtaji wa uwekezaji wa Dola Bilioni 1.18, ikifuatiwa na Uganda wenye uwekezaji wa dola za kimarekani 700
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Godffrey Mwambe amesema nchi ya Kenya inashika nafasi ya Tatu wakiwa na uwekezaji wa dola za kimarekani 670 na hivyo kuiweka Tanzania kuwa juu ya nchini zingine Afrika Mashariki.
Mwambe amesema kuwa Tanzania inaongoza kuvutia wawekezaji kutokana na mapinduzi makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ambapo hadi sasa imewekeza jumla ya miradi mipya 905 katika sekta mbalimbali nchini miradi ambayo itatengeneza ajira 115,055 kwa watanzania na kuleta tija na manufaa kwa taifa
Alisema kuwa katika kipindi hiki cha miaka mitatu TIC imeweza kuvutia wawekezaji na kuweza kuandikisha, mfano kuanzishwa kwa viwanda mbalimbali ambavyo vimeweza kuongeza pato la Taifa.
Akifafanua zaidi anasema kuwa baadhi ya miradi mikubwa zaidi iliyowekezwa nchini ni pamoja na ikiwemo kiwanda cha Goodwill Ceremics Ltd kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani kinachojihusisha na utegenezaji vigae na kimewekeza jumla ya dola za kimarekani milioni 53, huku kikitoa ajira za moja kwa moja 1500 kwa watanzania na ajira zisizo za moja kwa moja 3,000.
Tanzania imeendela kuweka rekodi ya kuvutia wawekezaji kwa nchi zilizopo ukanda wa Afrika Mashariki kwa kuwa na mtaji wa uwekezaji wa Dola Bilioni 1.18, ikifuatiwa na Uganda wenye uwekezaji wa dola za kimarekani 700
Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Godffrey Mwambe amesema nchi ya Kenya inashika nafasi ya Tatu wakiwa na uwekezaji wa dola za kimarekani 670 na hivyo kuiweka Tanzania kuwa juu ya nchini zingine Afrika Mashariki.
Mwambe amesema kuwa Tanzania inaongoza kuvutia wawekezaji kutokana na mapinduzi makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano ambapo hadi sasa imewekeza jumla ya miradi mipya 905 katika sekta mbalimbali nchini miradi ambayo itatengeneza ajira 115,055 kwa watanzania na kuleta tija na manufaa kwa taifa
Alisema kuwa katika kipindi hiki cha miaka mitatu TIC imeweza kuvutia wawekezaji na kuweza kuandikisha, mfano kuanzishwa kwa viwanda mbalimbali ambavyo vimeweza kuongeza pato la Taifa.
Akifafanua zaidi anasema kuwa baadhi ya miradi mikubwa zaidi iliyowekezwa nchini ni pamoja na ikiwemo kiwanda cha Goodwill Ceremics Ltd kilichopo Mkuranga Mkoani Pwani kinachojihusisha na utegenezaji vigae na kimewekeza jumla ya dola za kimarekani milioni 53, huku kikitoa ajira za moja kwa moja 1500 kwa watanzania na ajira zisizo za moja kwa moja 3,000.

Mkurugenzi Mkuu wa Kituo cha Uwekezaji (TIC) Godffrey Mwambe akisisitiza jambo kwa Waandishi wa Habari (Hawapo pichani), wakati wa mkutano wake na Waandishi wa Habari kueleza mafanikio ya TIC ndani ya Miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano, Mkutano ulifanyika leo Disemba 5, 2018 katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dar es Salaam.

: Waandishi wa Habari wakimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa TIC,Godffrey Mwambe (Kushoto) wakati wa Mkutano wake kueleza mafanikio ya TIC ndani miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Tano, Mkutano ulifanyika leo katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO Jijini Dar es Salaam.
Hivyo makala Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki
yaani makala yote Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/tanzania-kinara-wa-kuvutia-wawekezaji.html
0 Response to "Tanzania Kinara wa Kuvutia Wawekezaji Afrika Mashariki"
Post a Comment