Loading...
title : BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA
link : BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA
BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA
Aliyekuwa Mwalimu Wa Shule ya Msingi Buhororo iliyopo Wilayani Ngara, Mkoani Kagera na Mwanahabari Marehemu Shabani Ndyamukama, amezikwa kwao Kijiji Kagoma Wilayani Muleba Jana Aprili 6, 2019.
Marehemu Shabani (49) ambaye mpaka umauti unamkuta mbali na Taaluma yake ya Ualimu, alitambulika zaidi kama mwanahabari huku akiripotia Vyombo mbali mbali vikiwemo Redio, Magazeti na Globu za kijamii kazi aliyoifanya kwa umakini na ustadi Mkubwa. Mwanahabari huyu mbali na kile kinachosemwa kuwa kifo chake kimesababishwa na Shinikizo la damu, siku za hivi karibuni alikaririwa akiwa ameandika katika moja ya mitandao ya kijamii kuhusu maradhi yake yaliyokuwa yakimsumbua kubwa akitaja Msongo Wa mawazo uliosababishwa na kuugua kwa baadhi ya jamaa Wa karibu yake.
Hadi mauti yanamkuta Marehemu Shabani alizidiwa ghafla akiwa Jijini Mwanza katika Semina na Mafunzo kwa wanahabari ambapo Juhudi za kumpeleka hospitali zilifanyika na bahati mbaya akaaga Dunia. Marehemu ameacha mjane na watoto wanne wote Wa kiume.
Shabani Ndyamukama, enzi za uhai wake
Hivyo makala BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA
yaani makala yote BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/04/buriani-mwanahabari-shabani-nassib.html
0 Response to "BURIANI MWANAHABARI SHABANI NASSIB NDYAMUKAMA"
Post a Comment