Loading...

Kitilya, wenzake kizimbani tena leo

Loading...
Kitilya, wenzake kizimbani tena leo - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Kitilya, wenzake kizimbani tena leo, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Kitilya, wenzake kizimbani tena leo
link : Kitilya, wenzake kizimbani tena leo

soma pia


Kitilya, wenzake kizimbani tena leo


Grace Gurisha

Harry Kitilya na wenzake wawili
ALIYEKUWA Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Harry Kitilya, na wenzake wawili, leo wanatarajiwa kupandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakati kesi inayowakabili ya uhujumu uchumi itakapotajwa.

Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha anayeisikiliza, baada ya Hakimu Mkazi Emmilius Mchauru aliyekuwa akiisikiliza awali kuhamishiwa kwenye Mahakama nyingine.

Awali, upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ili kuukamilisha, kwa sababu kesi hiyo ni pana na inahitaji muda wa kupeleleza kwa sababu upelelezi utatakiwa kufanyika nje ya nchi.

Kitilya na wenzake wanaendelea kuwa rumande, ambapo hivi sasa wanatimiza mwaka mmoja gerezani kwa sababu ya upelelezi kutokamilika na pia wanashitakiwa kwa kutakatisha fedha, hivyo kisheria kukosa dhamana.

Mbali na Kitilya, wengine aliyekuwa mlimbwende wa Tanzania mwaka 1996, Shose Sinare na aliyekuwa mwanasheria wa benki ya Stanbic Tanzania, Sioi Solomon.

Kitilya na wenzake walipandishwa kizimbani mara ya kwanza kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam Aprili mosi, mwaka jana wakishitakiwa kula njama, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu, kughushi na kutakatisha fedha haramu.

Tangu siku hiyo kila kesi hiyo ikija mahakamani, upande wa Jamhuri umekuwa ukiiambia Mahakama kuwa upelelezi haujakamilika na kuomba tarehe nyingine ya kutajwa, ambapo mawakili wa washitakiwa hao wamekuwa wakipiga kelele kuhusu wateja wao kusota gerezani.

Hali hiyo ilisababisha, Wakili Alex Mgongolwa kuomba wateja wake waachwe huru, na wakishakamilisha upelelezi ndipo wakamatwe tena kuliko kukaa gerezani bila sababu, baada ya kushindikana hilo, wakaomba Serikali iwaeleze hatua waliyofikia, lakini bado hawajaeleza.

Awali, upande wa mashitaka ulidai mahakamani kuwa katika tarehe tofauti kati ya Agosti 2012 na Machi 2013 Dar es Salaam, washitakiwa hao watatu walipanga kwa kushirikiana na watu wengine ambao hawakufikishwa mahakamani hapo, kutenda kosa la kujipatia fedha kwa udanganyifu kutoka serikalini.

Ilidaiwa kuwa kati ya Agosti 2, 2012 kwenye makao makuu ya Stanbic Tanzania Limited, Kinondoni, Sinare akiwa na nia ovu, alighushi taarifa ya maombi ya fedha ya benki ya Standard ya Agosti 2, 2012.


Hivyo makala Kitilya, wenzake kizimbani tena leo

yaani makala yote Kitilya, wenzake kizimbani tena leo Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Kitilya, wenzake kizimbani tena leo mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/kitilya-wenzake-kizimbani-tena-leo.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Kitilya, wenzake kizimbani tena leo"

Post a Comment

Loading...