Loading...
title : Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/-
link : Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/-
Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/-
Jemah Makamba
MKAZI wa Kimara, Dar es Salaam, Dastan Mpea (28), amefikishwa kwenye Mahakama ya Wilaya ya Ilala akidaiwa kuiba Sh milioni 10 ndani ya gari namba T150 DBP mali ya Masudi Abdallah.
Akisoma mashitaka dhidi yake jana mbele ya Hakimu Mfawidhi Ritha Tarimo, mwendesha mashitaka Ashura Mnzava alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Desemba 7 mwaka jana akiwa barabara ya Libya, Ilala.
Alidai kuwa alivunja gari hilo na kuiba fedha zilizokuwamo huku akijua ni kosa na kinyume cha sheria za nchi.
Mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo ambapo mwendesha mashitaka alidai upelelezi wa kesi hiyo haukuwa umekamilika na kuiomba Mahakama iwapangie tarehe nyingine huku mshitakiwa akishindwa masharti ya dhamana na kurudishwa rumande.
Hivyo makala Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/-
yaani makala yote Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/- Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/- mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/kizimbani-kwa-wizi-wa-milioni-10.html
0 Response to "Kizimbani kwa wizi wa milioni 10/-"
Post a Comment