Loading...
title : TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO
link : TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO
TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO
Na Ramadhan K. Dau
Siku ya Jumatano tarehe 24 Mei 2017 ni siku ambayo itakumbukwa na Watanzania wengi na haswa Waislamu kwa kuondokewa na mzee wetu Alhaj Kitwana Selemani Kondo maarufu “KK” au mzee wa mjini.
Ilipofika siku ya Jumatano tarehe 24 Mei nikapata taarifa kupitia moja ya kundi sogozi (chat group) kuwa mzee KK amefariki dunia. Pamoja ya kuwa hali hiyo ilikuwa tayari inatawala fikra zangu lakini kifo hakizoeleki.
Moja kati ya sifa zake nyingi ni ujasiri. Mzee KK hakuwa mwoga na alikuwa na ujasiri wa kusimamia jambo ambalo anaamini ni sahihi na lina manufaa kwa nchi yetu. Mifano iko mingi. Kwa leo itoshe tu kuwa alisimamia suala la upatikanaji wa Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro kwa kujenga hoja kwa Rais wa wakati huo Mhe Benjamin William Mkapa mpaka Mhe Rais akashawishika kuwa ni jambo jema kuanzishwa kwa chuo hicho kwenye majengo ya kilichokuwa Chuo cha Mafunzo cha TANESCO.
(Pichani ni Mhe Mkapa akiwa na KK kushoto kwake na viongozi wengine waliohudhuria sherehe ya kuzindua uanzishwaji wa Chuo cha Kiislamu Morogoro).
(Pichani ni Mhe Mkapa akiwa na KK kushoto kwake na viongozi wengine waliohudhuria sherehe ya kuzindua uanzishwaji wa Chuo cha Kiislamu Morogoro).
Kama kuna mtu mmoja ambaye ametoa mchango wa kipekee uliopelekea upatikanaji wa Chuo Kikuu cha Waislamu cha Morogoro (MUM) mtu huyo ni mzee Kitwana Kondo.
Kwa kuenzi jitihada zake hizo, na kwa kuzingatia mzee Kondo ni Mwenyekiti mwanzilishi wa Taasisi ya Maendeleo ya Waislamu (MDF), taasisi ambayo ndiyo Mmiliki wa MUM, nashauri uongozi wa Chuo utafute jengo lenye hadhi pale Chuoni lipewe jina lake. Kwa siku za usoni, Chuo kitakapoanza kutoa shahada za Uzamivu (PhD), nashauri mzee Kitwana Kondo atunukiwe PhD (Honoris Causa) posthumously.
Hivyo makala TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO
yaani makala yote TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/taazia-obituary-buriani-mzee-kitwana.html
0 Response to "TAAZIA (OBITUARY) BURIANI MZEE KITWANA KONDO"
Post a Comment