Loading...
title : KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI
link : KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI
KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI
Taasisi ya Karimjee Jivanje (KJF) imeongeza nguvu zaidi katika kuhifadhi na kusimamia mazingira ya bara la Afrika kwa kudhamini wanafunzi kutoka Tanzania kuendelea na masomo yaliyopendekezwa ya shahada ya uzamili katika eneo hilo.
Mwenyekiti wa heshima wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee nchini Tanzania, Hatim Karimjee alisema mpango huo wa masomo uliundwa na taasisi na mpaka sasa imejitolea kudhamini wanafunzi wawili mwaka 2016 na wanne mwaka huu.
Alisema Taasisi imetoa msaada wa dola 105,000 sawa na ( 236.2Millioni Tzs) mwaka jana ambapo wanafunzi wawili walichukua kozi ya shahada ya uzamili, na mwaka huu wanafunzi wanne wamedhaminiwa na taasisi ambapo imetoa msaada wa dola 210,000 sawa na (472.5 Miilioni Tzs) na ina mpango wa kutoa dola 180,000 sawa na (405Million Tzs) kwa ajili ya kudhamini nafasi za masomo mwaka ujao “Karimjee Jivanjee imefurahi kuzindua nafasi za masomo ya uhifadhi wa mazingira.
Wanafunzi hawa watajifunza masomo yalipondekezwa ya shahada ya uzamili ya usimamizi wa uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori katika bara la Afrika. Tunapenda kushirikiana na chuo kikuu cha Glasgow nchini Scotland na chuo cha Sayansi na Teknolojia cha Nelson Mandela kilichopo Arusha kuanzisha masomo ya shahada ya uzamili ambapo wanafunzi watasoma mwaka mmoja Glasgow na mwaka mmoja Mkoani Arusha. Wanafunzi hao watatambulika kama wanafunzi kutoka Karimjee,”
Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee, Hatim Karimjee (kulia) akimkabidhi kifaa cha kusomea mmoja wa mwanafunzi aliyepata udhamini wa kusoma shahada ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori katika bara la Afrika Zabibu Kabalika (kushoto) katika hafla iliyofanyika mkoani Arusha.
Mwenyekiti wa kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua masomo yaliyopendekezwa ya kozi ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori mkoani Arusha, Nyuma Kulia ni Dr. Haydon wa chuo kikuu Glasgow kilichopo Scotland, akifuatiwa na Prof, Karoli Njau wa chuo cha sayansi na teknolojia cha Nelson Mandela, wengine ni wanafunzi waliopata nafasi ya masomo, Zabibu Kabalika (wa tatu kulia) na Evaline Munisi.
Mwenyekiti wa Kundi la makampuni ya Karimjee Jivanjee akizungumza wakati wa hafla fupi ya kuzindua kozi ya uzamili iliyopendekezwa katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori mkoani Arusha. kulia ni wanafunzi waliopata nafasi ya masomo ya shahada ya uzamili katika uhifadhi wa mazingira ya wanyamapori Evaline Munisi ( kwanza kulia) na Zabibu Kabalika.
Hivyo makala KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI
yaani makala yote KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/karimjee-jivanje-yadhamini-wanafunzi.html
0 Response to "KARIMJEE JIVANJE YADHAMINI WANAFUNZI KATIKA KOZI YA UZAMILI YA UHIFADHI WA MAZINGIRA YA WANYAMAPORI"
Post a Comment