Loading...
title : Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja.
link : Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja.
Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja.
Na Maryam Kidiko-Maelezo Zanzibar. 16/08/2017.
NAIBU Waziri wa Afya Harusi Said Suleiman amewataka Walinzi wa Hospitali ya Mnazi Mmoja kubadilika katika utendaji wa kazi zao ili kuongeza mashirikiano kati yao na wananchi wanaokwenda kwa ajili ya kupata huduma mbali mbali katika hospitali hiyo
Hayo aliyasema katika Hospitali ya Mnazi Mmoja kwenye Mafunzo ya Siku moja ya Walinzi wa Hospitali hiyo ambayo yanalengo la kuongeza ufanisi wa utendaji kazi zao na kuongeza Mashirikiano na wateja wao.
Aliwaeleza walinzi hao kuwa kumekuwa na malalamiko kwa baadhi ya walinzi wamekuwa wakitumia lugha mbaya kwa wagonjwa na wananchi wanaofika kuangalia wagonjwa wao jambo ambalo sio zuri.
Aliwasisitiza walinzi wa Hospitali ya Mnazimmoja kutumia lugha nzuri kwa Wagojwa kwani kufanya hivyo itapelekea kujenga mashirikiano katika utendaji mzima wa kazi yao.
Alisema kunatofauti kubwa kati ya ulinzi wa Hospitali na ulinzi katika sehemu nyengine kwani mara nyingi wananchi wanaofika Hospitali wanahitaji kuhurumiwa kutokana na mazingira wanayokuwa nayo.
“Walinzi wetu tunawaamini sana na tunajuwa mnakumbana na changamoto nyingi lakini ni lazima mtumie akili za ziada ili Wagojwa wanapofika wajiskie furaha hatakama wapo katika huzuni,”Alisema Naibu Waziri.
Hata hivyo alishauri zinapotokea Changamoto ndogo ndogo kuzishughulikia kwa njia nzuri za ushirikiano kwa pande zote zinazohusika .
Aidha aliwaeleza walinzi hao kuwa baada ya kupata mafunzo hayo Serikali haitawavumilia kuona wanaenda kinyume na utaratibu uliowekwa katika kuwahudumia wananchi.
Mkurugenzi Utawala na Uendeshaji wa Hospitali ya Mnazimmoja Abubakar Khamis Hamadi alisema lengo la mafunzo hayo ni kuongeza mashirikiano mazuri kati ya Wagojwa, wananchi wanaofika kwa ajili ya kuangalia wagonjwa na Walinzi.
Alieleza matumaini yake kuwa mafunzo hayo yatawawezesha Walinzi kujuwa njia sahihi za kuwashuhulikia wateja wao wanapofika katika Hospitali na kujuwa wajibu wao.
“ Tunapata malalamiko mengi kutoka kwa Wagojwa hivyo tumeamuwa kutowa mafunzo hayo kwa Walinzi ili kuondoa matatizo na kuongeza mashirikiano mazuri baina yao,” alisema Mkurugenzi huyo.
Aliwataka walinzi waliopata mafunzo hayo kuyafanyia kazi ili kutimiza lengo la mafunzo yenyewe na kuleta ufanisi katika kazi yao bila kutokea malalamiko mengine.
Mkurugenzi Abuubakar amewaomba Wananchi wanaofika hospitalini hapo kutowa mashirikano mazuri kwa Walinzi na iwapo litatokezea tatizo wafike katika kitengo cha huduma kwa Mteja kwa lengo la kushughulikiwa.
Msaidizi Mkuu wa Walinzi Aboubakar Hassan Bakari aliahidi baada ya mafunzo hayo watabadilika na kuwashauri walinzi wenzake kuwa waadilifu huku wakijua wao ni kampuni ya ulinzi ya Kibiashara hivyo wanatakiwa kuvutia waajiri wao.
Mmoja wa Walinzi waliopata mafunzo hayo Mwanaidi Mriha Nasibu alishukuru kupata mafunzo hayo ambayo yatawasaidia kutatuwa Changamoto zilizopo baina yao na Wagojwa.
Hivyo makala Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja.
yaani makala yote Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja. mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/08/uongozi-wa-hospitali-za-serikali-wapewa.html
0 Response to "Uongozi wa Hospitali za Serikali Wapewa Mafunzo ya Huduma Kwa Wateja."
Post a Comment