Loading...

DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE

Loading...
DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE
link : DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE

soma pia


DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE


Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika Kituo cha Forodha Bandarini, kilichoko katika Bandari ya Dar es Salaam na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, kufanya mabadiliko makubwa ya watumishi walioko katika idara ya upimaji na ukaguzi wa mizigo baada ya kubainika kuwa baadhi yao wanajihusisha kwa namna moja au nyingine na upotevu wa mapato ya Serikali.

Dokta Mpango ametoa muda wa siku saba kwa TRA kumpa taarifa kamili ya utekelezaji wa maagizo hayo, ikiwemo kuwahamisha watumishi wote waliokaa muda mrefu kwenye eneo hilo la upimaji na ukaguzi wa mizigo ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato ya Serikali katika Bandari hiyo.

Ameshangazwa na kitendo cha Mapato katika Bandari ya Dar es Salaam kutoongezeka licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, kuboresha Bandari hiyo kutokana na baadhi ya watumishi wasio waaminifu kushirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kodi ya serikali.
Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kulia) akiwa katika kikao na Maafisa Waandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) alipofanya ziara ya kukagua utendaji ambapo aliwataka kuchukua hatua dhidi ya watumishi wasiowaaminifu wanaolikosesha Taifa mapato stahiki.
Meneja wa Idara ya Forodha, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bandari ya dar es Salaam, Bw. John Micah (kulia) na Meneja anaye husika na suala la Mafuta Bw. Stephen Malekano (kushoto) wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (hayupo pichani) alipofanya ziara Idara ya Forodha, Bandarini, Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa Maafisa waandamizi wa Mamlaka ya mapato Tanzania-TRA, alipofanya ziara ya kushitukiza bandari ya Dar es Salaam na kuagiza kitengo cha ukaguzi na upimaji wa mizigo bandarini kifumuliwe baada ya watumishi wake kutofanyakazi ya kukusanya mapato ya Serikali ipasavyo
Afisa Kitengo cha Bandari Majahazi, Bw. Mahmood Makame, akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) kuhusu changamoto ya elimu kuhusu masuala ya kodi kwa wateja wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kushitukiza katika ofisi hiyo.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango).



Hivyo makala DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE

yaani makala yote DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/09/dokta-mpango-aagiza-watumishi-wa-tra.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE"

Post a Comment

Loading...