Loading...

Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi....

Loading...
Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi.... - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi...., tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi....
link : Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi....

soma pia


Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi....

Mwambawahabari 

Aliyekuwa Naibu Waziri wa TAMISEMI, Seleman Jafo baada ya kuteuliwa na kuapishwa kuwa Waziri wa wizara hiyo amewaahidi Watanzania kuwa wategemee utendaji mzuri wa kazi kutoka kwake huku akiwaomba watumishi wote umma kufanya kazi kwa spidi.

Wakizungumza Ikulu jijini Dar es salaam mara baada ya kuapishwa, Mhe Jafo amesema lengo lake ni kuisukuma nchi ifikie malengo yanayotarajiwa huku Dkt Kigwangalla akisema Mh. Rais ameonyesha imani kubwa sana na uwezo wake.

“Kikubwa zaidi niwaahidi Watanzani wategemee utendaji mzuri wa kazi, lakini niombe sana watumishi wote wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lazima wajipange kufanya kazi kwa bidii , Wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya, Wakurugenzi naomba waongeze spidi na Wakurugenzi waongeze spidi lakini watumishi wote waongeze spidi lengo ni tuisukume nchi yetu ifike katika malengo tunayoyatarijia

Hata hivyo Mhe. Jafo alipoulizwa kuwa ikiwa ni miongoni mwa Waziri walipandishwa yeye anafikiri ni kwanini kapandishwa na kuwa Waziri kamili? Akajibu “Ni mipango ya mwenyezi Mungu jambo la kwanza, la pili ni imani ya Mheshimiwa Rais kwangu, tatu ni utendaji wa kazi kwasababu ni lazima popote utakapo niweka ni lazima nifanye kazi kwasababu nina dhamana ya Watanzania naamini popote Mungu ananiona.”

Kwa upande wake aliyekuwa Naibu Waziri wa Afya ambaye kwasasa ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamisi Kigwangalla amesema kuwa “nimefarijika sana pia nimepewa imani kubwa na Mhe. Rais, nimepewa Wizara nyeti ni wizara ambayo inachangia asilimia 17.2 ya pato la taifa ni wizara nyeti sana, na mimi kupewa jukumu hili maana yake mhe. Rais ameonyesha imani kubwa sana na uwezo wangu lakini pia na uzalendo nilionao naomba niwaambie Watanzania na Mhe. Rais Kuwa sitawaangusha.”


Hivyo makala Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi....

yaani makala yote Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi.... Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi.... mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/10/baada-ya-kuapishwa-jafo-na-dkt.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Baada ya kuapishwa Jafo na Dkt Kigwangalla wasema hivi...."

Post a Comment

Loading...