Loading...
title : UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA
link : UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA
UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA
Mkuu wa Mkoa wa Mtwara leo amezindua rasmi zoezi la Usajili na Utambuzi wa Watu kwa wananchi wa mkoa huo tayari kuanza rasmi kwa zoezi la usajili kwa wananchi ikihusisha kuchukuliwa picha, saini na alama za Kibaiolojia.
Akizungumza katika uzinduzi huo Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mhe. Evod Mmanda kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa amesema Mkoa wa Mtwara umejipanga na uko tayari kwa zoezi hilo, na kuahidi kutoa ushirikiano kwa hali na mali kuhakikisha hakuna mwananchi yeyote mwenye sifa ambaye ataachwa bila kusajiliwa.
Katika sherehe za uzinduzi rasmi wa zoezi hilo zilizofanyika makao makuu ya Mkoa huo Mtwara; zilihudhuriwa na Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya, Meya, Katibu Tawala Mkoa, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri zote, Makatibu Tawala wa Wilaya, Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama ngazi ya Mkoa, Watumishi katika ngazi mbalimbali na vyombo vya Habari.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara mjini akikata utepe kuashiria uzinduzi rasmi zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, wakati wa uzinduzi wa zoezi hilo uliofanyika katika ukumbi wa mikutano katika ofisi ya mkuu wa Mkoa wa Mtwara na kuhudhuriwa na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, watumishi wa NIDA pamoja na wageni wengine waalikwa.
Baadhi ya Wakuu wa Wilaya na watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa pichani wakisikiliza jambo kutoka kwa mwakilishi Mkuu wa mkoa wa Mtwara wakati wa sherehe ya uzinduzi wa zoezi la Usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara
Baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa mkoa wa Mtwara pamoja na wageni waalikwa wakiwa katika ukumbi wa mikutano kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa wa Mtwara wakati wa zoezi la uzinduzi wa usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa wananchi wa mkoa wa Mtwara
Afisa usajili msaidizi wa NIDA Ndg. Fredy Mahundi akifanya zoezi la usajili kwa mara ya kwanza kwa mwananchi wa mkoa wa Mtwara mara baada ya zoezi la uzinduzi wa usajili kwa wananchi wa Mkoa wa Mtwara kukamilika.
Bi Amina Bakari akichukuliwa alama zake za Vidole ambapo alipata nafasi ya kuwa mwananchi wa kwanza kusajiliwa kwa mkoa wa Mtwara mara baada ya zoezi la uzinduzi wa usajili wa Vitambulisho vya Taifa kwa mkoa wa Mtwara kukamilika.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA
yaani makala yote UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/11/uzinduzi-wa-zoezi-la-usajili-wa.html
0 Response to "UZINDUZI WA ZOEZI LA USAJILI WA VITAMBULISHO VYA TAIFA WAFANYIKA MKOANI MTWARA"
Post a Comment