Loading...
title : WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA
link : WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA
WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega ameteketeza Nyavu haramu 242 zenye thamani ya Sh Mil.242 baada ya wavuvi kuzisalimisha wenyewe katika kisiwa cha Zilagula kilichopo halmshauri ya Buchosa wilayni Sengerema mkoani Mwanza.
Akizungumza wakati wa uteketezaji wa nyavu hizo, Ulega aliwapongeza wavuvi hao kwa hatua hiyo walioichukua huku akikazia msimamo wa serikali wa kupambana na uvuvi halamu. Pamoja na kuwapongeza huko,Ulega aliwasisitiza wavuvi hao kuzingatia sheria na taratibu za uvuvi ili kuzilinda rasilimali hiyo, ambayo ilikuwa inaelekea kutoweka.
"Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa samaki, wazazi walikuwa wamebaki asilimia nne, wenye hadhi ya kuvuliwa kwa maana ya sentimita 50 hadi 85 wamebaki asilimia tatu na wachanga wamebaki asilimia 93, na kama uvuvi huu ungeendelea maana yake ziwa lingebaki jangwa," alisema Ulega
Waziri Ulega aliwataka wavuvi hao kununua nyavu zinazokubalika kwenye viwanda ambavyo vinauza nyavu hizo, badala ya kuendelea kutumia nyavu zisizoruhusiwa kwani watapata hasara kwa kuteketezewa na wengine kushtakiwa kwa mujibu wa sheria.
kwa upande wake kiongozi kazi maalumu mkoa wa kioparesheni Sengerema, Charles Lwekaza alisema baada ya kufanya operesheni hiyo iliyoanza mapema Januari mwaka huu, baadhi ya wavuvi waliamua kuzisalimisha nyavu hizo wenyewe bila shuruti.
Akizungumza wakati wa uteketezaji wa nyavu hizo, Ulega aliwapongeza wavuvi hao kwa hatua hiyo walioichukua huku akikazia msimamo wa serikali wa kupambana na uvuvi halamu. Pamoja na kuwapongeza huko,Ulega aliwasisitiza wavuvi hao kuzingatia sheria na taratibu za uvuvi ili kuzilinda rasilimali hiyo, ambayo ilikuwa inaelekea kutoweka.
"Kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa samaki, wazazi walikuwa wamebaki asilimia nne, wenye hadhi ya kuvuliwa kwa maana ya sentimita 50 hadi 85 wamebaki asilimia tatu na wachanga wamebaki asilimia 93, na kama uvuvi huu ungeendelea maana yake ziwa lingebaki jangwa," alisema Ulega
Waziri Ulega aliwataka wavuvi hao kununua nyavu zinazokubalika kwenye viwanda ambavyo vinauza nyavu hizo, badala ya kuendelea kutumia nyavu zisizoruhusiwa kwani watapata hasara kwa kuteketezewa na wengine kushtakiwa kwa mujibu wa sheria.
kwa upande wake kiongozi kazi maalumu mkoa wa kioparesheni Sengerema, Charles Lwekaza alisema baada ya kufanya operesheni hiyo iliyoanza mapema Januari mwaka huu, baadhi ya wavuvi waliamua kuzisalimisha nyavu hizo wenyewe bila shuruti.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akiongoza shughuli za kuteketeza Nyavu haramu 242 zenye thamani ya Sh Mil.242 baada ya wavuvi kuzisalimisha wenyewe katika kisiwa cha Zilagula kilichopo halmshauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza
.Wavuvi wakisogeza Nyavu haramu 242 zenye thamani ya Sh Mil.242 eneo la kuchomea baada ya kuzisalimisha wenyewe katika kisiwa cha Zilagula kilichopo halmshauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega akizungumza na wavuvi katika kisiwa cha Zilagula kilichopo halmshauri ya Buchosa wilayani Sengerema mkoani Mwanza.Picha na Emanuel Massaka.
Hivyo makala WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA
yaani makala yote WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/01/wavuvi-waaswa-kuzingatia-sheriataratibu.html
0 Response to "WAVUVI WAASWA KUZINGATIA SHERIA,TARATIBU ZA UVUVI KUZILINDA RASILIMALI ZIWA VICTORIA"
Post a Comment