Loading...

Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi

Loading...
Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi
link : Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi

soma pia


Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi

Na Greyson Mwase, Pwani
Wilaya za Mkuranga, Kibiti na wilaya ya Rufiji katika kata ya  Ikwiriri zimeanza  kupata nishati ya uhakika ya umeme mara baada ya kuunganishwa katika Gridi ya Taifa na kukamilika kwa kituo cha kupozea umeme cha Mbagala kilichopo jijini Dar es Salaam.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani wakati akizungumza na wananchi wa Ikwiriri wilayani Rufiji mkoani Pwani katika ziara yake ya siku moja jana (tarehe 22 Machi, 2018) ya kukagua miundombinu ya umeme iliyounganishwa na Gridi ya Taifa kutokea katika kituo cha kupoza umeme cha Mbagala hadi Ikwiriri na kufuatilia utekelezaji wa miradi ya usambazaji wa umeme vijijini inayosimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
Dkt. Kalemani alisema lengo la kuunganisha wilaya hizo na Gridi  ya taifa ni kuhakikisha wananchi wanapata nishati ya umeme wa uhakika na kuondokana na umeme unaotokana na mitambo ya mafuta ya Somangafungu  ambayo imekuwa ikiharibika mara kwa mara.
Alisema awali kabla ya wilaya hizo kuunganishwa na Gridi ya Taifa, kulikuwepo na changamoto ya kukatika kwa umeme katika wilaya hizo kutokana na mitambo kuhitaji matengenezo ya mara kwa mara.
Alisema ili kukabiliana na changamoto hiyo, Serikali iliamua kuunganisha  wilaya hizo kwenye Gridi ya Taifa ili kuwepo na umeme wa uhakika ambao mbali na matumizi ya majumbani unategemewa na viwanda  vilivyopo katika mkoa wa Pwani
Katika hatua nyingine akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kinyanya kilichopo katika wilaya ya Kibiti mkoani Pwani ambapo aliwasha rasmi umeme, Waziri Kalemani aliwataka wakandarasi wanaosambaza umeme vijijini kupitia REA kuhakikisha vijiji vyote na  vitongoji vyake vinapata umeme wa uhakika.
 Mhandisi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Temeke, Mhandisi Alex Adam (wa pili kushoto) akielezea shughuli zinazofanywa na kituo cha kupoza umeme cha Mbagala kwa Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (katikati) katika ziara hiyo.
 Mafundi wa kampuni ya Sengerema Engineering wakikamilisha ujenzi wa miundombinu ya umeme kwa ajili ya kuingizwa kwenye Gridi ya Taifa katika kijiji cha Kinyanya kilichopo wilayani Kibiti mkoani Pwani.
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani (kulia) akibonyeza kitufe kuashiria uwashaji wa umeme katika kijiji cha Kinyanya kilichopo wilayani Kibiti mkoani Pwani.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi

yaani makala yote Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/03/mkuranga-kibiti-ikwiriri-zaanza-kupata.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Mkuranga, Kibiti, Ikwiriri zaanza kupata umeme wa Gridi"

Post a Comment

Loading...