Loading...

Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation

Loading...
Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation
link : Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation

soma pia


Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation

Na Mwandishi Wetu
Zabron Mbwaga ambaye ni Mzalishaji mbegu, aliyepo Viwanja vya NaneNane, Njiro mkoani Arusha ametwaa tuzo ya mshindi wa jumla wa tuzo za Ujasiriamali ya Citi Foundation. Tuzo hiyo inaambatana na fedha taslimu dola za Marekani 7,500.

Mbwaga ambaye aliwezeshwa upanuzi wa shughuli zake kwa mikopo kutoka BRAC Tanzania, alianza kazi zake akiwa na mtaji wa shilingi milioni 2 kabla ya kuongezewa nguvu na BRAC.

Tuzo hizo zilizofanyika mwishoni mwa wiki zilitolewa kwa wajasiriamali 16 na ofisa mikopo mmoja.

Mshindi wa pili ni Anney Sekulasa akiondoka na dola za Marekani 6000 huku mshindi wa tatu ni Lydia Majoro ambaye aliondoka na dola za Marekani 4000. Nafasi ya mjasiriamali mlemavu ilitwaliwa na Aneth Geraw aliyepata dola za Marekani 2000.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Tanzania Microfinance Association (TAMFI), Joel Mwakitalu (kulia) akikabidhi cheti kwa mshindi wa tatu wa tuzo za Ujasiriamali za Citi Foundation, Lydia Majoro wakati wa hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mjasiriamali mlemavu aliyefanya vyema Aneth Geraw ambaye aliondoka na kitita cha dola za Marekani 2000 wakati hafla ya kukabidhi tuzo za ujasiriamali za Citi Foundation zilizofanyika jijini Dar es Salaam
 Mkurugenzi Mtendaji wa CITI Bank, Joseph Carasso (kulia) akikabidhi cheti kwa mshindi wa pili wa tuzo za Ujasiriamali za Citi Foundation, Anney Sekulasa (kushoto) katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es Salaam. Anayeshuhudia tukio hilo katikati ni Mkurungenzi wa Fedha na Masoko wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Alexander Mwinamila.
 Mkurugenzi Mtendaji wa CITI Bank, Joseph Carasso (kulia) na Mkurungenzi wa Fedha na Masoko wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Alexander Mwinamila (katikati) kwa pamoja wakikabidhi cheti kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Yetu Microfinance, Attemius Millinga (kushoto) ambapo taasisi yake imekuwa na ubunifu mkubwa wa bidhaa zake sambamba na mifumo ya kutolea huduma na methodolojia wakati wa hafla fupi ya tuzo za ujasiriamali za Citi Foundation zilizofanyika jijini Dar es Salaam.
 Mwanamke aliyefanya vyema kwenye ujasiriamali mdogo, Lucy Kiongosi akipozi baada ya kupokea cheti kilichoambatana na dola za Marekani 2000 wakati wa hafla ya tuzo za ujasiriamali za Citi Foundation zilizofanyika mwishoni wa wiki jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mkurungenzi wa Fedha na Masoko wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Alexander Mwinamila na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa CITI Bank, Joseph Carasso.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation

yaani makala yote Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/04/mzalishaji-mbegu-apata-tuzo-ya.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Mzalishaji mbegu apata Tuzo ya Ujasiriamali ya Citi Foundation"

Post a Comment

Loading...