Loading...

MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI

Loading...
MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI
link : MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI

soma pia


MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI

*Ni katika kesi inayomkabili Halima Mdee

Na Karama Kenyunko, Blogu ya jamii
MKUU wa Upelelezi Wilaya ya Ilala (RCO), Davis Msangi ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa hajawahi kumuhoji Rais John Magufuli jinsi anavyojisikia kuhusu maneno yaliyotamkwa na mbunge wa Kawe Halima Mdee dhidi yake.

RCO Msangi ameyaeleza hayo leo mahakamani hapo wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba alipokuwa akijibu swali la Wakili wa utetezi Peter Kibatala.

Katika kesi hiyo, Mdee anakabiliwa na shtaka la kumtoa lugha chafu kwa Rais Dk. John Magufuli.

Akimuhoji shahidi huyo,Wakili Kibatala alimuuliza Msangi kama anamfahamu Rais John Magufuli na anaishi wapi. alijibu kuwa anaishi Ikulu. Pia alimuuliza shahidi huyo kama aliwahi kwenda kumuhoji jinsi anavyojisikia kuhusu maneno yanayodaiwa kutamkwa na Mdee kwa sababu yeye ndiyo muhanga.

RCO Msangi alijibu kuwa hajawahi kwenda kumuhoji wala hakutumia taratibu zozote za kumuhoji.

 RCO Msangi katika ushahidi wake amedai kuwa hafahamu msimamo wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusiana na kauli ya Rais Magufuli kuhusu watoto wa kike waliopata mimba shule wasirudishwe shule.

Pia RCO Msangi alipoulizwa kwamba Mdee alikaa muda gani chini ya ulinzi, amedai kuwa sio kwa zaidi ya Saa  48, ambapo alifikishwa Polisi July 4,2018 ila tarehe kuondoka haijui.

Baada ya shahidi huyo kumaliza kuhojiwa na Wakili Kibatala, Hakimu Simba amesema kesi hiyo imeshatimiza mwaka mmoja na ilipaswa iwe ishatolewa hukumu, ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi  August 7 na 8, 2018 ili kuendelea na ushahidi.

Katika kesi hiyo Mdee anadaiwa Julai 1 3 mwaka 2017 katika Makao Makuu ya Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) iliyopo mtaa wa Ufipa wilaya ya Kinondoni ni kuwa  Rais John Magufuli  “anaongea hovyohovyo , anatakiwa  afungwe breki”  na kwamba kitendo ambacho kingeweza  kusababisha uvunjifu wa Amani.


Hivyo makala MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI

yaani makala yote MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/mkuu-wa-upelelezi-ilala-aulizwa-kama.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "MKUU WA UPELELEZI ILALA AULIZWA KAMA ANAPAFAHAMU ANAPOISHI RAIS MAGUFULI"

Post a Comment

Loading...