Loading...

WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI

Loading...
WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI
link : WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI

soma pia


WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali haina mpango wa kununua madeni yaliyosababishwa na mikopo ya kibenki kwenye vyama vikuu vya ushirika nchini.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo (Jumamosi, Julai 7, 2018) wakati akizungumza na wanaushirika na mamia ya wakazi wa Jiji la Mwanza waliohudhuria maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Furahisha, jijini humo.

“Serikali ya awamu ya tano hatuna biashara ya kununua madeni ya vyama vikuu, kulikuwa na tabia ya watu wa ushirika kukopa na hali ikiwa mbaya wanakimbilia Serikalini. Serikali hii hatuna biashara hiyo,” amesema.

Waziri Mkuu amesema anazo taarifa kwamba Chama Kikuu cha mkoa wa Kagera (KCU) kimekopa fedha Benki ili kiweze kulipa deni la mwaka 2014. “Nimeambiwa KCU wamekopa fedha benki ili kulipa deni la mwaka 2014, hii inaingia akilini kweli? Mnakopa fedha kulipa deni la zamani, ni kwa nini msiwatafute waliosababisha deni na kuwachukulia hatua?,” alihoji.

“Ninyi mlikuwa watu sita ambao mlikubaliana kama viongozi, mlienda kukopa kuzidi uwezo mlionao. Leo hii ni kwa nini serikali ije kulipa wakati mmetumia ninyi?,” aliuliza Waziri Mkuu.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya awamu ya tatno inasisitiza masuala ya ushirika kwa sababu imeamua kuwahudumia wananchi kuanzia ngazi ya chini kuanzia pembejeo, dawa hadi masoko.

“Tunataka tuondoe utaratibu wa chama kikuu kukopa fedha benki ili kikanunue mazao. Vyama vingi vimetengeneza hasara, leo hii vyama vikuu vina madeni. Hii ni kwa sababu mlikopa fedha benki wakati hata hamjui mna kilo ngapi ambazo zimevunwa.
 Waziri Mkuu, Kassim  Majalawa akizungumza katika Maadhimisho ya siku ya ushirika dunianiyaliyofanyika kitaifa  kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
 Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba akizungumza wakati alipomkaribisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa  Furahisha jijini Mwanza, Julai 7, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea kutoka kwa Mwenyekiti wa Shirikisho la Ushirika nchini, Bibi Renata Mwageni (kushoto) Tuzo ya  Rais John Pombe Magufuli iliyotolewa na Wanaushirika nchini  ili kutambua mchango wa Rais  katika kuendeleza sekta ya ushirika na kuinua uchumi wa wananchi wa Tanzani ya 2018 . Makabidhiano hayo yalifanyika kwenye  Maadhimisho ya Siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye  uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Juni 7, 2018.  Wapili kushotoi ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na kulia ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab  Telack.
 Baadhi ya wananchi waliohudhuria katika Maadhimisho ya  Siku ya Ushirika duniani  wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati alipohutubia kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mizani ya Kielektroniki ya kupima uzito wa pamba wakati alipotembelea banda la Chama Kikuu  cha Ushirika cha Nyanza katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa  Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Wapili kulia ni Waziri wa Kilimo, Dkt. Charles Tizeba na watatu kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwaanjelwa.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  akitazama pamba iliyostawi vizuri wakati alipotembelea banda la Chama Kikuu cha Ushirika cha Nyanza  baada ya kuhutubia katika maadhimisho ya siku ya Ushirika Duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018.  Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama samaki waliokaushwa  wakati alipotembelea banda la Vyma vya Ushirika katika Soko la Kimataifa la Kirumba – Mwaloni wilayani Ilemela baada ya kuhutubia katika Maadhimisho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa Furahisha jijini Mwanza Julai 7, 2018. Kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula ambaye pia ni Mbunge wa Ilemela .
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na watumishi wa TANESCO wakati alipotembelea banda lao katika maonyesho ya siku ya Ushirika duniani yaliyofanyika kitaifa kwenye uwanja wa furahisha jijini Mwanza  Julai 7, 2018.  Wapili kushoto ni Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack na watatu kushoto ni Naibu Waziri wa Kilimo, Dkt. Mary Mwanjelwa.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI

yaani makala yote WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/waziri-mkuu-serikali-haitanunua-madeni.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAZIRI MKUU: SERIKALI HAITANUNUA MADENI"

Post a Comment

Loading...