Loading...

Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka

Loading...
Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka
link : Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka

soma pia


Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka


Na.WAMJW,Bungeni,Dodoma
Idadi ya wanachama wachangiaji wa mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya imeongezeka kutoka wanachama 164,708 waliokuwa wameandikishwa  mwaka 2001/2002 hadi wanachama 873,012 mwezi Septemba 2018.
Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu wakati akiwasilisha  taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mfuko huo kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Bungeni jijini Dodoma.
“Ongezeko hili limetokana na kanuni na misingi  inayotumika katika kuendesha utaratibu wa mfuko huu ikiwa ni pamoja na uchangiaji wenye usawa kwa kuzingatia viwango vya mshahara,usawa katika kupata huduma na ushiriki wa Serikali katika usimamizi kwa faida ya wanachama” alisema Waziri Ummy.
Waziri Ummy amesema kuwa kwa upande wa Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF), jumla ya kaya zilizojiunga hadi Septemba mwaka huu ni 2,220,953 ikiwa ni sawa na wanufaika wapatao 13,506,330 sawa na asilimia 25 ya watanzania wote’ kwa hiyo mifuko hii yote inatoa huduma kwa watu 17,656,697 sawa na asilimia 33 ya watanzania wote kwa mujibu  wa idadi ya makadirio ya watanzania kwa sasa.Idadi ya wanufaika imeongezeka  kutoka 691,774 mwaka 2001/2002 hadi wanufaika 4,150,367 sawa na asilimia 8 ya watanzania wote” alisema Waziri Ummy.
Aidha, Waziri Ummy amesema kuwa mpaka sasa idadi ya wanachama wengi waliojiunga  asilimia 67 ni watumishi wa umma ambao wanajiunga kwa mujibu wa sharia.
Hata hivyo Waziri Ummy alisema mfuko unaendelea kutoa elimu na kubuni vifurushi mbalimbali vitakavyovutia wananchi wengi kujiunga na kufaidika  na mfuko ambapo utawawezesha wanachama wengi zaidi kujiunga hasa wale wa sekta isiyo rasmi na kujiwekea malengo ya kuwafikia watanzia asilimia 50 mwaka 2020.
“Mfuko umekamilisha uandaaji wa vifurushi vya michango na mafao kulingana na uwezo wa wananchi kulipia bima  ya afya,suala hili lipo katika hatua za mwisho kabla ya kuanza kwa utekelezaji”. Alisisitiza Waziri Ummy.
Waziri Ummy amesema kuwa mpango huo utamwezesha mwananchi kuchagua vifurushi vya aina mbalimbaliu vya huduma  anayoitaka kwa utaratibu utakaojulikana kama ‘JIPIMIE’ na wanachama watalipa kidogo kidogo kwa utaratibu ujulikanao kama ‘DUNDULIZA’ ambao tayari umeshakamilika.
 
 Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia,Wazee na Watoto Ummy Mwalimu akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa shughuli za mfuko wa Bima ya Afya(NHIF) kwenye kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo  jijinini Dodoma ambapo alisema wachangiaji wa mfuko huo wameongezeka kutoka wanachama 164,706 mwaka 2001/2002 hadi wanachama 873,012 septemba mwaka huu.
IMG-20181024-WA0025
Mkurugenzi wa NHIF Bw.Bernad Konga akijibu maswali kutoka kwa wajumbe wa kamati ambapo alisema mfuko wake upo tayari kuanza mara moja kutoa huduma kupitia vifurushi vipya vitakavyojulikana kama JIPIMIE ili watanzania waweze kupata huduma za matibabu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya nchini
IMG-20181024-WA0028
Wakurugenzi wa NHIF wakipitia taarifa ya mfuko huo wakati ikiwasilishwa kwenye kamati mapema leo
IMG-20181024-WA0030
Katibu Mkuu Afya Dkt.Mpoki Ulisubisya(wa kwanza kulia),Mkurugenzi wa NHIF Bw.Benard Konga(anayefuata)pamoja na wakurugenzi  wengine wa Wizara na NHIF wakifuatilia taarifa hiyo.
IMG-20181024-WA0032
.WazirinUmmy Mwalimu akifafanua jambo mbele ya kamati ya kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii leo jijini Dodoma.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA>>>


Hivyo makala Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka

yaani makala yote Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/10/idadi-wa-wachangiaji-wa-mfuko-wa-bima.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Idadi wa wachangiaji wa Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF)waongezeka"

Post a Comment

Loading...