Loading...
title : MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI
link : MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI
MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
WATU wamefurika katika nyumba ya kuhifadhia maiti Chimoro Nairobi kutambua miili ya ndugu zao waliouwawa katika shambulio la kigaidi lililotekelezwa na kundi la Al shabab.
Rais Uhuru Kenyatta amehutubia taifa na kueleza kuwa watu 14 wamefariki katika shambulio hilo huku watu zaidi ya watu 700 wakiokolewa.
Kenyatta ameeleza kuwa operesheni hiyo imekamilika na waliotekeleza shambulio hilo wameuwawa na amewahakikishia usalama wakenya wote huku wanasiasa wakizuiliwa kuingia mahali hapo.
Aidha umoja wa Afrika (AU) na Marekani kupitia balozi wao nchini humo Robert Gidec wamelaani vikali tukio hilo la kigaidi lililogharimu maisha ya wengi.
Pia imeelezwa kuwa kamera za usalama (CCTV) zimenasa video ambayo inaonesha magaidi wanne wakiingia katika viunga vya hoteli hiyo na maafisa wa polisi wamegundua nyumba iliyokuwa mita chache kutoka eneo la tukio ambayo inasadikika kutumika kwa kupanga mbinu hizo za uvamizi.
Chanzo: The StandardMedia
Hivyo makala MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI
yaani makala yote MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/01/mamia-wajitokeza-mochwari-kutambua.html
0 Response to "MAMIA WAJITOKEZA MOCHWARI KUTAMBUA JAMAA ZAO NAIROBI"
Post a Comment