Loading...
title : ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA
link : ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA
ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA
Na Woinde Shizza Globu ya jamii Arusha
Timu ya mpira Wa miguu ya mkoani Arusha ijulikanayo kwa jina la Arusha United (wana utalii), Leo imetangaza rasmi kujitoa katika mashindano ya ligi daraja la kwanza Tanzania bara kwa kile kichodaiwa vurugu za Mara kwa Mara zinazotokea katika ligi hiyo.
Akizungumza na waandishi wa habari Murugenzi mtendaji wa timu hiyo Otte Ndauka alisema kuwa timu hiyo imeamua kujitoa rasmi katika mashindano hayo kutokana na vurugu wanazofanyiwa Mara kwa Mara viwanjani wakati wakicheza michezo mbalimbali.
Alisema kuwa timu yao ya Arusha United imefanyiwa vurugu katika mechi mbalimbali ikiwemo mchezo nambari 69 Wa ligi daraja LA kwanza uliochezwa mjini Tabora mnamo February 2 mchezo uliochezwa katika kiwanja cha All Hassan Mwinyi.
"Mchezo huu tulienda tulifika sikumoja kabla kwa mujibu Wa sheria tulitakiwa kufanya mazoezi kwa ajili ya mchezo husikalakini jambo LA kusikitisha sana na lisilo lakiugwana viongozi Wa Rhino Rangers kwa kushirikiana na Meneja Wa uwanja walifanya kula jitiada kuhakikisha hatufanyi mazoezi,Aisha pia katika mechi ingine tuliocheza na kilabu ya Polisi pia tulifanyiwa vurugu na sio timu tu au wachezaji wanafanyiwa vurugu hapana lakini pia waandishi wetu wanapigwa na hata kunammoja aliaribiwa vifaa vyake vya Kazi" alisema Ndauka.
Alisema kuwa matukio yote ambayo yametokea wameandika barua TFF kulalamika pamoja na Bodi ya ligi lakini hakuna uamuzi wowote Wa kinithamu ambalo wameuchukua hivyo ndio maana wameamua kujitoa katika ligi hiyo.
Kuhusiana na swala La mikataba ya wacheza pamoja na Mali za klabu hiyo walisema kuwa bodi ya timu hiyo inakaa chini na wachezaji kujadili kuhusiana na mikataba hiyo pia wanampango Wa kuketi na bodi kujadili kuhusiana na Mali hizo.
Akizungumzia suala hilo Katibu wa chama cha mpira Wa miguu mkoa Wa Arusha Zakayo Mjema alisema kuwa wao kama chama cha mpira Wa miguu Mkoa Wa Arusha awajapata taarifa yoyote kuhusiana na timu hiyo kujitoa

Mkurugenzi mtendaji Wa timu ya Arusha United (WANAUTALII) Otte Ndauka
Hivyo makala ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA
yaani makala yote ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/03/arusha-united-yajitoa-rasmi-ligi-daraja.html
0 Response to "ARUSHA UNITED YAJITOA RASMI LIGI DARAJA LA KWANZA"
Post a Comment