Loading...
title : TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
link : TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO








Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato, Eliud Mwaiteleke akijadiliana jambo na na Kaimu Mkurugenzi wa Masoko wa NHC, Itandula Gambalagi.









Wakifuatilia hafla hiyo.

Wakiagana mara baada ya kuhitimisha hafla ya uzinduzi wa mauzo ya viwanja.
Halmashauri ya Wilaya ya Chato ikishirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) inautangazia umma juu ya uuzaji wa viwanja 1,035 vilivyopimwa na kuwekewa barabara katika eneo la Mlimani na Rubambangwe kata ya Muungano. Mauzo ya viwanja yanaanza wiki ijayo.
Wananchi wote mnakaribishwa kununua viwanja vyenye matumizi mbalimbali kama vile makazi, makazi na biashara, viwanja vya biashara, maeneo ya kumpumzikia, viwanja vya michezo na huduma mbalimbali za kijamii kama zahanati, Shule, Vituo vya Mafuta kwa bei ya kuanzia Tsh 1,300 kwa mita ya mraba.
Viwanja vipo mita chache kutoka katikati ya mji wa Chato. Vipo mkabala na barabara kuu iendayo Bukoba. Pembezoni mwa Ziwa Victoria.
Viwanja vilivyopimwa na kupangwa kwa ajili ya makazi vina ukubwa kama ifuatavyo:
1. Ujazo wa juu (High density)
2. Ujazo wa kati (Medium density)
3. Ujazo wa chini (Low density)
VIWANGO VYA GHARAMA YA VIWANJA KWA MATUMIZI MBALIMBALI
1. Makazi –Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,300/=
2. Makazi na biashara- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 1,700/=
3. Biashara (Hotel, Vituo vya mafuta, maduka makubwa)- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
4. Huduma za jamii (Zahanati, shule ya awali, sekondari) Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
5. Ibada/kuabudu- Bei ya kiwanja kwa mita moja ya mraba ni Shilingi 2,200/=
UTARATIBU WA KUNUNUA KIWANJA
Chukua fomu ya maombi kutoka ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Chato au Ofisi ya NHC iliyo karibu nawe.
Lipia angalau asilimia 30 ya thamani ya kiwanja unachonunua na kiasi kinachobaki kilipwe ndani ya siku 90.
Malipo yote yafanyike kwenye akaunti ya benki ifuatayo: Jina la Akaunti : MRADI WA VIWANJA CHATO Nambari ya akaunti : 327 100 116 07 Benki: NMB Tawi la Chato
Rejesha fomu ya maombi uliyojaza kwa usahihi ukiambatanisha pamoja na vielelezo vinavyohitajika ikiwemo nakala ya malipo (deposit slip) kutoka benki.
Utapatiwa barua ya uthibitisho (Offer Letter) mara tu ombi lako litakapokubaliwa, pamoja na masharti ya kukamilisha malipo ya kiwanja unachochagua.
Kwa maelezo zaidi tembelea ofisi za Idara ya ardhi ya Halmashauri ya Wilaya ya Chato.
Au KAMBARAGE House, 1 Mtaa wa Ufukoni, Dar es Salaam, Tanzania. Kwa Mawasiliano piga namba +255 282 228 007/ +255 754 444 333.
PHILIP SHONI
KWA NIABA YA MKURUGENZI MTENDAJI
HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
21/02/2019
Hivyo makala TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO
yaani makala yote TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/02/taarifa-kwa-umma-kuhusu-uuzaji-wa.html
0 Response to "TAARIFA KWA UMMA KUHUSU UUZAJI WA VIWANJA KATIKA ENEO LA RUBAMBANGWE HALMASHAURI YA WILAYA YA CHATO"
Post a Comment