Loading...
title : NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA
link : NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA
NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA
Na Kumbuka Ndatta,Arusha
NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdalla Ulega ametembele taasisi za Serikali zilizopo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na wadau wengine wa sekta ya mifugo na uvuvi.
Akitoa taarifa fupi kwa Naibu waziri,Mkurugenzi wa Wakala wa vyuo vya Mafunzo ya Mifugo (LITA) Kampasi ya Tengeru Joseph Msemwa amemweleza Ulega kuwa kazi kubwa ya LITA ni kutoa mafunzo ya muda mrefu na muda mfupi,kufanya utafiti na ushauri elekezi na uzalishaji Mali.
Pia mafunzo hayo yamejikita katika fani ya afya ya mifugo na uzalishaji.Aidha mafunzo hayo yanalenga kutoa watalaam wenye ujuzi wa hali ya juu katika fani za ufugaji.Amesema lengo ni kuwa na mtazamo wa Kujiajiri na kuendesha miradi mbalimbali ya kibiashara.
Msemwa amemwambia Naibu Waziri baadhi ya changamoto zinazoikabili Kampasi hiyo kuwa ni uchakavu wa majengo,huduma duni za maji,upungu wa watumishi na Muundo wa Wakala.Kwa upande wa Mtendaji Mkuu wa LITA (CEO)Magreth Pallangyo pamoja na kupokea maagizo kutoka kwa Naibu Waziri,ameahidi kuyatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na kuyashughukia ipasavyo.
Akihutubia watumishi waliofika katika ukumbi wa Kampasi ya Tengeru Ulega amesema kuwa vyuo hivi vya mafunzo ya mifugo ndio nguzo mama katika kuchochea maendeleo ya uchumi wa Taifa letu."Wakufunzi wa Vyuo hivi vya Mifugo jitahidi sana kuhusianisha kile mnachokifundisha darasani na mazingira halisi ya itanzania.
"Toeni elimu bora ili muweze kuwasaidia vijana hawa na taifa kwa ujumla.Vijana hawa wakitoka hapa tunataka waone kuwa wamezungukwa na fursa za kiuchumi," amesema Ulega.
Mkufunzi mwandamizi wa kitengo cha teknolojia ya maziwa,Theresia Teti akimwelezea Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega namna ya usindikaji wa maziwa jijini Arusha.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi,Abdallah Ulega akiangalia namna ya uhimilishaji unavyofanyoka katika kituo cha Taifa cha(NAIC) kilichopo Usa River jijini Arusha.Picha na Emmanuel Massaka,MMG Arusha)
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akitembelea shamba la samaki Shazan lililopo jijini Arusha.
Hivyo makala NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA
yaani makala yote NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/naibu-waziri-wa-mifugo-na-uvuvi-afanya.html
0 Response to "NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI AFANYA ZIARA MKOANI ARUSHA"
Post a Comment